BURUNDI YACHUNGUZA MIILI ILIYOPATIKANA ZIWANI
Mamlaka kaskazini mwa Burundi zimeanzisha uchunguzi baada ya mifuko
yenye miili ya binaadam kupatikana ikielea katika ziwa Rweru lililopo
kwenye mpaka na Rwanda. Wavuvi katika eneo hilo wamesema
miili ya watu wasiofahamika imekuwa ikionekana katika ziwa hilo katika
wiki za hivi karibuni. Haifahamiki watu hao walikufa katika mazingira
gani. Polisi nchini Rwanda wametoa taarifa ikikanusha kuwa miili hiyo ni
ya raia wake waliouawa na kutupwa ziwani.
